Psalms 18:10-15


10 aAlipanda juu ya kerubi akaruka,
akapaa juu kwa mbawa za upepo.

11 bAlifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika,
hema lake kumzunguka,
mawingu meusi ya mvua ya angani.

12 cKutokana na mwanga wa uwepo wake
mawingu yalisogea,
ikanyesha mvua ya mawe
na umeme wa radi.

13 d Bwana alinguruma kutoka mbinguni,
sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.

14 eAliipiga mishale yake na kutawanya adui,
naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.

15 fMabonde ya bahari yalifunuliwa,
na misingi ya dunia ikawa wazi
kwa kukaripia kwako, Ee Bwana,
kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.

Copyright information for SwhKC